Quantcast
Channel: Millard Ayo
Viewing all articles
Browse latest Browse all 31461

Ligi ya Mabingwa barani ulaya yaanza .

$
0
0

champs leag

Michuano mikubwa kwa ngazi ya vilabu duniani UEFA Cahmpions League ilianza rasmi hapo jana ambapo viwanja nane barani humo vilishuhudia timu 16 zikivaana .

Kocha wa Manchester United David Moyes akiwa anaiongoza Manchester United kwenye ligi ya mabingwa kwa mara yake ya kwanza aliweza kupata ushindi wa 4-1 dhidi ya Bayer Leverkusen .

Mshambuliaji Wayne Rooney alikuwa nyota wa mchezo akifunga mabao mawili na kutengeneza bao lingine lililofungwa na Antonio Valencia huku Robin Van Persie naye akifunga bao moja . Mabao mawili ya Bayer Leverkusen yalifungwa na Simon Rolfes na Beki Omer Toprek .

champs leagg

Ushindi mkubwa kuliko yote kwa usiku wa jana (Jumanne) ulikuwa nchini Uturuki ambako Cristiano Ronaldo aliwaongoza Real Madrid kupata ushindi wa 6-1 mbele ya wenyeji wao Galatasaray . Ronaldo alifunga mabao matatu peke yake huku Isco , Karim Benzema wakifunga mabao mengine . Umut Bulut alifunga bao pekee la Galatasaray .

Paris St Germain wanaocheza michuano hii kwa msimu wao wa pili mfululizo waliwafunga Olympiakos  4-1 katika mchezo uliopigwa nchini Ugiriki.

champs leagggggg

Mabingwa watetezi wa michuano hii Bayern Munich waliwafunga CSKA Moscow 3-0 . Mabao ya Bayern yalifungwa na David Alaba , Arjen Robben na Mario Mandzukic .

Man City wakiwa ugenini nchini Poland walishinda mchezo wao dhidi ya Viktoria Plzen kwa   3-0 . Yaya Toure,Edin Dzeko na Sergio Aguero ndio walifunga mabao ya City kwenye mchezo huo .

champs leaggg

Katika mchezo mwingine Benfica waliwafunga Anderletch 2-0 , Shakhtar Donetsk wakashinda ugenini dhidi ya Real Sociedad na Juventus na Fc Copenhagen walitoka sare ya 1-1 .

 

Matokeo ya mechi za Ligi ya mabingwa .

Manchester United 4-2  Bayer Leverkusen .

Galatasaray             1-6  Real Madrid.

Real Sociedad         0-2  Shakhtar Donetsk .

Fc Copenhagen       1-1  Juventus .

Olympiakos             1-4  Paris St Germain.

Benfica                    2-0  Anderletch.

Viktoria Plzen          0-3 Manchester City

Bayern Munich        3-0 CSKA Moscow.

 

Michuano hiyo itaendelea hii leo ambapo Arsenal watakuwa wageni wa Olympique Marseile , Napoli watacheza na Borrusia Dortmund , Fc Barcelona watakipiga na Ajax Amsterdam , Ac Milan watacheza na Glasgow Celtic , Chelsea watakipiga na Fc Basel , Atletico Madrid watakuwa mzigoni na Zenith St Petersburg , Schalke wakicheza na Steua Bucharest  huku Austria Wien wakicheza na Fc Porto.

 

 Ratiba ya Mechi za Leo.

Chelsea  vs  Fc Basel .

Schalke  vs  Steua Bucharest.

Olympique Marseile  vs  Arsenal.

Napoli vs Borrusia Dortmund .

Atletico Madrid vs Zenith St Petersburg .

Fc Barcelona vs Ajax Amsterdam.

Ac Milan vs Glasgow Celtic.

Austria Wien vs Fc Porto

Story Za Michezo Kwa Hisani Ya Benki Ya NMB.

 

Use Facebook to Comment on this Post


Viewing all articles
Browse latest Browse all 31461